MAN U KUPAMBANA BILA NYOTA WAKE ALHAMISI HII
Hofu imetanda kwa mashabiki wa klabu ya Machester United ya nchini Uingereza kuelekea katika mchezo wao wa Nusu fainali ya Europa League ambao utakaofanyika siku ya Alhamisi. United katika mchezo wake wa kwanza wa nusu fainali, huenda ikawakosa wachezaji wake Nyota wa kikosi cha kwanza cha Mreno Jose Mario dos Santos Mourinho, wachezaji hao wakiwa ni pamoja na Bailly , Chris Smalling paomoja na Phil Jones. Wengine ambao wapo katika hati hati ya kukosekana ni Zlatan Ibrahimovic, Marcos Rojo na Timothy Fosu-Mensah Mchezaji ghali zaidi duniani kwa sasa, Paul Pogba anatarajiwa kurejea katika mchezo huo, utakaofanyika nchini Hispania baada ya kukosa mechi mbili kutokana na kuwa majeruhi.