Posts

Showing posts from March, 2017

ZANZIBAR RASMI MWANACHAMA KAMILI WA CAF

Image
Hatimaye mkutano mkuu wa 39 wa Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) unaoendelea mjini Addis-Ababa, Ethiopia, umepitisha ombi la chama cha soka Zanzibar (ZFA) kuwa mwanachama rasmi wa CAF. Ni jambo la kihistoria kwa Zanzibar kwani safari hii ombi lao limepitishwa bila kupingwa na inakuwa nchi ya 55 mwanachama wa kujitemea wa CAF. Awali Zanzibar ilikuwa inaunganishwa na Tanzania bara chini ya TFF na kupelekea kukosa haki za kushiriki kama nchi kwenye mashindano yanayoandaliwa na CAF pamoja na yale ya FIFA. Pendekezo hilo lilipelekwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ndugu, Jamal Malinzi na lilipokelewa na wajumbe 54 wengine waliokuwepo. Hii maana yake ni kuwa kwa sasa CAF ndio shirikisho mwanachama wa FIFA kwa upande wa mabara lenye wanachama wengi zaidi kuliko wote. Vilabu vya Zanzibar vimekuwa vikishiriki mashindano mbalimbali ya CAF lakini kwa ngazi ya kitaifa hawakuwa na ruhusa na walicheza kwa kuungana na Tanzania bara na kushiriki kama Tanzania. Kwa maana ...

HAYATOU APIGWA BAO NA AHMD AHMAD URAIS CAF

Image
Rais wa chama cha soka cha Madagascar Ahmad Ahmad ameushtua ulimwengu wa soka baada ya kumbwaga Issa Hayatou ambaye alikuwa rais wa muda mrefu wa shirikisho la soka Barani Afrika na kushinda urais wa Caf. Uchaguzi uliomalizika Addis Ababa umempa ushindi Ahmad Ahmad baada ya kupata kura 34 dhidi ya 20 za Issa Hayatou. Matokeo hayo yanahitimisha miaka 29 ya utawala wa Hayatou kama kiongozi wa juu wa soka la Afrika.Mipango na mbinu kabla ya uchaguzi zimepelea kuwashangaza wengi baada ya kushuhudia kambi ya Hayatou ikidondoshwa. Hayatou mwenye miaka 70 sasa, alikuwa rais wa CAF tangu mwaka 1988 wakati huo Lionel Messi akiwa na miezi tisa tu tangu azaliwe wakati mtawala huyo mzaliwa wa Cameroon alipotangazwa kusimamia soka la bara la Afrika. Alianza kutawala tangu March 10, 1988 alikuwa anaifukuzia rekodi ya kuendelea kusalia madarakani kwa awamu ya nane mfululizo.Uchaguzi ulifanyika leo baada ya mkutano mkuu wa 39 huko mjini Addis Ababa.Ahmad anakuwa rais wa saba wa CAF kwenye his...

PLUIJM AJIA KITANZI MIAKA MIWILI SINGIDA UNITED

Image
Baada ya picha kusambaa zikimuonesha kocha wa zamani wa Yanga Hans van der Pluijm akiwa na mchezaji mpya (Kutinyu) aliyesajiliwa na Singida United, hatimaye leo March 17, 2017 kocha huyo amesaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo ya mkoa wa Singida iliyopanda kucheza ligi kuu msimu ujao. Uongozi wa Singida United umetoa taarifa rasmi kwa umma kuthibitisha kumsainisha kocha huyo mkataba wa miaka miwili kuwa kocha mkuu wa timu hiyo.

MKUDE, AJIB WASAINI KANDARASI MPYA SIMBA SC

Image
Na Hussein Mkuwia Mwenyekiti wa usajili wa klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe unaweza ukasema amecheza kama Pele mara baada ya kukamilisha mipango ya usajili kwa Ibrahim Ajib na Jonas Mkude wachezaji waliokuwa wanaelekea mwisho mwa mikataba yao.  Wawili hao mikataba yao ilikuwa inaisha mwishoni mwa msimu huu lakini wamekubali kuongeza mikataba ya miaka miwili kila mmoja. Kwenye mikataba yote ya wachezaji hao, kila mchezaji anaruhusiwa kwenda kufanya majaribio kwenye klabu itakayoomba mchezaji husika kufanya hivyo na kuhama kama taratibu zitafuatwa. Hii Ni Habari nzuri kwa wapenzi wa klabu ya Simba kwani wachezaji hao ni nguzo kubwa klabuni hapo kwasasa.