MKUDE, AJIB WASAINI KANDARASI MPYA SIMBA SC
Na Hussein Mkuwia
Mwenyekiti wa usajili wa klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe unaweza ukasema amecheza kama Pele mara baada ya kukamilisha mipango ya usajili kwa Ibrahim Ajib na Jonas Mkude wachezaji waliokuwa wanaelekea mwisho mwa mikataba yao.
Wawili hao mikataba yao ilikuwa inaisha mwishoni mwa msimu huu lakini wamekubali kuongeza mikataba ya miaka miwili kila mmoja.
Hii Ni Habari nzuri kwa wapenzi wa klabu ya Simba kwani wachezaji hao ni nguzo kubwa klabuni hapo kwasasa.
Comments
Post a Comment