Posts

Showing posts from October, 2017

CHADEMA YAZADI KUWA KIVUTIO CHA MAWAZIRI

Image
Baada ya Mhe.Lazaro Nyarandu kuachana na CCM na kuomba kujiunga na Chadema,nimejaribu kukumbuka idadi ya mawaziri wakuu,mawaziri,manaibu waziri ambao wamehamia Chadema,kwa haraka nimepata idadi ipatayo nane akiwemo Lowassa,Sumaye,Kingunge,Ntagazwa,Makongoro,Lau Masha,Ole Medeye(baadaye alihamia UDP) na sasa Nyalandu. Hawa wote walipata kuongoza Wizara mbalimbali kwa vipindi tofauti. Pia mhe.Ruth Mollel huyu alikuwa Katibu Mkuu wa wizara na sasa yupo Chadema. Kwa hali ilivyo je idadi inweza kuongezeka? Maana wapo wanaomtaja Mhe. Nape kuwa yupo mbioni kuhama na wengine pia. Zipo habari kuwa Chadema wamekuwa wakipita pita na kujigamba kuwa watawachukua wastaafu wa vyombo vya ulinzi na usalama hasa wakitajwa viongozi wawili wa TISS, Apson Mwangonda na Hassy Kitine kuwa ni watu wao.

EZRA CHILOBA AJIONDOA TUME YA UCHAGUZI KENYA(IEBC)

Image
Afisa mkuu mtendaji wa tume ya uchaguzi nchini Kenya Ezra Chiloba anatarajiwa kuchukuwa likizo ya wiki tatu na hatoshiriki katika uchaguzi wa marejeo wa Alhamisi kulingana na gazeti la Daily Nation nchini Kenya. Kulingana na duru katika tume hiyo ya IEBC bwana Chiloba alifanya uamuzi huo wa kibinafsi wa kutoshiriki ili kujenga upya imani ya washikadau ambao wamelalamika kuhusu maafisa wa tume hiyo. Kulingana na gazeti hilo afisa huyo amekuwa chini ya shinikizo kubwa kutoka muungano wa upinzani Nasa kujiuzulu, huku mgombea wa urais wa muungano huo Raila Odinga akiitisha maandamano ya kumlazimisha kuondoka pamoja na maafisa wengine ikiwatuhumu kwa kusimamia vibaya uchaguzi wa Agosti 8 ambapo rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi. Matokeo ya uchaguzi huo hatahivyo yalifutiliwa mbali na mahakama ya juu ambayo iliamua kwamba haukufanyika kulingana na sheria. Kulingana na Daily Nation Bwana Chiloba anachukua likizo baada ya mwenyekiti wa tume hiyo wafula Chebukati kutaka maafi...

KOCHA WA RAYON SPORTS YA RWANDA NDIYE MRITHI WA MAYANJA SIMBA SC

Image
Klabu ya Simba leo Oktoba 19, 2017 imemtambulisha aliyekuwa kocha wa Rayon Sport ya Rwanda Masoud Djuma kuchukua nafasi ya Jackson Mayanja ambaye jana ametangaza kuachana na klabu hiyo.  Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara mchana wa leo amemtangaza Masoud Djuma kuchukua nafasi ya kocha msaidizi katika klabu yao hiyo ya Simba na kuwaomba wanachama wa mashabiki wa Simba kumpa ushirikiano kocha huyo.  " Tunawaomba wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba mumpe ushirikiano kocha wetu Masoud Djuma yeye ndiye atakuwa msaidizi wa Kocha Omog kuanzia leo Oktoba 19, 2017 na pia tumeboresha benchi la ufundi kwa kumteua meneja mpya Richard Robert yeye anachukua nafasi ya Dkt Kapinga ambaye alikuwa meneja kwa muda tuliokuwa naye mfupi lakini amerudi kwa mwajiri wake nasi klabu tumeona turidhie " alisema Haji Manara.  Mbali na hilo Manara amekanusha taarifa zinazoendelea kusambaa kwenye mitandao ya kija...

MAYANJA AITOSA SIMBA SC

Image
Kocha Msaidizi wa kikosi cha Simba Jackson Mayanja, leo amefikia uamuzi wa kujiuzulu nafasi yake kutokana na kuitaji muda zaidi wakwenda kushughulikia mambo ya kifamilia. Uongozi wa Simba umemruhusu kuweza kwenda kutatua matatizo ya kifamilia lakini pia imempatia baraka zote na kumtakia kila la kheri katika kazi yake ya kufundisha soka.

OKWI AIREJESHA SIMBA SC KILELENI LIGI KUU TANZANIA BARA

Image
Ligi kuu soka Tanzania Bara iliendelea tena hapo jana lakini macho na maskio ya wadau na wapenzi wasoka yalikuwa yameelekezwa huko katika Uwanja wa Uhuru ambapo mabingwa wa FA, Simba SC wakiwa wenyeji waliwakaribisha Mtibwa Sugar. Katika mchezo huo ambao ulikuwa nakasi na vuta nikuvute baina ya timu zote mbili wenyeji wa mchezo huo Simba walikubali kuruhusu bao la mapema katika kipindi cha kwanza dakika ya 37 likifungwa na nahodha wa Mtibwa Sugar, Stamili Mbonde kwa njia ya kichwa. Hadi dakika 90 za mchezo Mtibwa Sugar ilikuwa ikiongoza hali iliyopelekea hadi baadhi ya mashabiki wa Simba kukata tamaa na kuanza kuondoka Uwanjani. Katika dakika tatu za nyongeza mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uganda na klabu ya Simba, Emmanuel Arnold Okwi akaendeleza ufalme wake wa mabao baada ya kufunga goli lake la saba kwenye uwanja huo wa Uhuru na kuinusuru timu yake kupoteza kwa mara ya kwanza mechi ya ligi kuu msimu huu. Bao safi la Emmanuel Okwi lilipatikana baada ya kupiga faulo iliyo...

MLIPUKO WAUWA TAKRIBANI WATU 300 SOMALIA

Idadi ya watu waliouawa kwenye mlipuko mkubwa wa bomu katika eneo lenye shughuli nyingi kwenye mji mkuu wa Somalia Mogadishu siku ya Jumamosi, imefikia watu 300 hadi sasa, kwa mujibu wa ripoti ya shirika la hahari la Reuters Takriban watu wengine 300 walijeruhiwa kwa mujibu wa AFP, wakati lori lililokuwa limejazwa milipuko lilipolipuka karibu na lango la hoteli. Reuters walimnukuu Ahmed Ali, muuguzi anayefanya kazi kwenye hospitali moja akisema kuwa miili 160 haikuweza kutambuliwa na hivyo ilizikwa na serikali jana. Anasema kuwa miili mingini iliziwa na jamaa zao. Hilo ndilo shambulizi baya zaidi kutokea nchini Somalia tangu kundi la al-Shabab lianzishe harakati zake mwaka 2007. Rais Mohamed Abdullahi "Farmajo" Mohamed alilaumu kundi la al-Shabab kwa shambulizi hilo katili. "Tumethibitisha kuwa watu 300 waliuawa kwenye mipuko huo. Idadi ya waliokufa huenda bado ikaongezeka na kuna watu kadha ambao bado hawajulikani waliko," Abdikadir Abdirahman, mkurugenz...

LADY JAYDEE KUFUNGA NDOA NA SPICY

Image
Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Judith Wambula(Lady Jaydee) amesema suala la yeye kufunga ndoa na mpenzi wake Spicy watu waliache kama lilivyo kwani ni ishu ya maisha binafsi zaidi. Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘I Miss You’ ameiambia Planet Bongo ya EA Radio kuwa watu kutokuwa na haraka na suala hilo na haelewi ni kwanini amekuwa akiulizwa kila mara. “Kwanini watu wanapenda sana kupangia watu maisha, mgekuwa mnaacha vitu vinaflow , mtu kamaliza shule unanza kumuambia mbona hufanyi kazi wakati mtu labda ameomba kazi hajapata, unaulizwa mara unaolewa lini, unaulizwa unazaa lini waache watu waishi maisha yao, msitengemee vitu sana” amesema Lady Jaydee. “Watu walishakula ubwabwa na mambo yakashindikana vile vile, sasa husilazimishe kama mtu hajajiandaa kwanini mtake kulazimisha ubwabwa?. Wanapenda kumpangia mtu kitu afanye wakati hataenda kuishi naye mwisho wa siku mkumbuke haya ni maisha yangu, kwa hiyo nadhani tungeyaacha tukajikita kwenye muziki tu” a...

"UMALAYA SIO DILI" -GIGGY MONEY

Image
Msanii wa Bongo Fleva na Video Queen, Gigy Money amefunguka kuwa moja ya vitu anavyovichukia katika maisha yake ni umalaya huku akidai tabia hiyo inashusha hadhi ya mwanamke. Gigy Money na Amber Lulu wakiwa kwenye party ya mtoto wa Hamisa Mobetto. Gigy Money amesema anajua kuwa kuna wanawake wanaishi mjini kwa kazi hiyo lakini yeye hawezi kufanya kazi hiyo na ndio kazi anayoichukia maishani mwake. “ Nachukia sana kazi ya umalaya najua watu wengi hasa wasichana wengi wanaifanya na wanaipenda ila haina faida kubwa, faida yake ni ya muda mfupi, “amesema Gigy Money kwenye mahojiano yake na Bongo5 kwenye sherehe ya Mtoto wa Hamisa Mobetto. Hata hivyo, Gigy Money amekiri wazi kuwa alishawahi kudanga kipindi cha nyuma lakini kwa sasa ameacha tabia hiyo.

MKE WA DEO FILIKUNJOMBE ANENA KUHUSU MUMEWE

Ikiwa ni miaka miwili imepita tangu aliyekuwa Mbunge wa Ludewa Deo Haule Filikunjombe afariki dunia, mke wa wake Sarah Habiba amesema Tanzania ina pengo kubwa kwa kumpoteza Deo. Kwenye ukurasa wake wa instagram, Sarah Habiba ameandika ujumbe huo, wakiadhimisha miaka miwili ya kifo chake kwa kufanya ibada takatifu. "Mume wangu leo umefikisha miaka miwili tangu upatwe na mauti, kiukweli umeacha pengo kubwa kwa watanzania, jamii na familia kiujumla, watoto wako wanakumiss sana, mimi mkeo, Mungu akulaze mahala pema peponi mpenzi wangu, ntakukumbuka daima mpenzi", ameandika Sarah Habiba. Deo Filikunjombe alifariki octoba 15, 2015 kwa ajali ya helkopta akitokea Dar es salaam kwenda Ludewa, na kuanguka kwenye msitu wa mbuga ya Selous, akiwa na rubani wake William Silaa ambaye ni baba mzazi wa Jerry Silaa, na msaidizi wa Deo Filikunjombe, Bwana Mkwera. Deo Filikunjombe atakumbukwa kwa uchapa kazi wake na juhudi alizozionyesha kwenye kamati ya Bunge kuibua sakata la Escrow akiwa n...

BUNGE LAFANYA KIKAO NA FAMILIA YA LISSU

Image
Wakati Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiendelea na  matibabu katika Hospitali ya Nairobi , familia yake imefanya kikao cha siri na uongozi ya Bunge kujadili matibabu ya mbunge huyo. Kikao hicho kimefanyika leo Jumatatu jijini Dar es Salaam na imeelezwa kimehudhuriwa na Spika Job Ndugai, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, Katibu wa Bunge, Thomas Kashilila, Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, Mbunge wa Hanang’, Dk Mary Nagu na ndugu watatu wa Lissu, wanaume wawili na mwanamke mmoja. Baada ya kupata taarifa za uwepo wa kikao hicho  Blacknationtz blog  iliweka kambi nje ya Ofisi Ndogo za Bunge tangu saa 3:55 asubuhi na kushuhudia shughuli za kawaida zikiendelea huku kukiwa na watu wachache wanaoingia na kutoka ndani ya ofisi hizo. Ilipofika saa 7:40 mchana, alitoka Mbatia akielekea kwenye gari lake baada ya kumaliza kikao hicho. Mwandishi alimfuata kujua kilichojiri ndani ya kikao hicho, Mbatia alikiri kuwepo kwa kikao hicho lakini hakutaka kuzungumza l...

DIAMOND ASITISHA HUDUMA ZA AFYA AMANA

Image
Mwanamuziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz amesherehekea siku yake ya kuzaliwa leo kwa kutembelea hospitali ya Amana ambako amesababisha shughuli zisimame kwa muda. Katika ziara yake hiyo aliyoifanya leo Jumatatu, Diamond ametoa vifaa tiba vyenye thamani ya Sh4 milioni. Muda wote aliokuwa hospitalini hapo wagonjwa na waliokuwa wakiwahudumia walitoka kwa ajili ya kumuona msanii huyo. Diamond ambaye sasa  anatamba na ngoma yake ya Hallelujah , amesema alifikia uamuzi wa kutembelea kwenye hospitali hiyo kwa kuwa ndipo mahali alipozaliwa. Amesema anajivunia kuwa na watu wazuri wa karibu ambao wanamshauri kurudisha kwenye jamii inayomzunguka. "Najua hospitali kuna mahitaji mengi nikaona kwa uwezo wangu mdogo nami nishiriki kusaidia mahali nilipozaliwa siku ya leo ili nipate pia fursa ya kuwaona watoto waliozaliwa tarehe kama yangu," "Nafahamu kuna changamoto nyingi, niwasihi watu wengine waangalie ni namna gani wanaweza kusaidia," amesem...