Posts

Showing posts from 2018

ANGALIA CHEGE CHIGUNDA ALICHOFANYA KWA NANDY

Image

VIWANDA VYA KOROSHO KUJENGWA NCHINI

Image
SERIKALI imo katika mchakato wa kuanzisha kiwanda cha korosho Mkuranga, Mtwara na Tunduru katika mwendelezo wa juhudi za kuwa na Tanzania ya uchumi wa kati na ya viwanda. Tanzania inazalisha tani 260,000 za korosho kwa mwaka na sasa ina viwanda 12 vya ubanguaji. Akizungumza Dar es Salaam jana juu ya umuhimu wa kuacha utaratibu wa kusafirisha korosho ghafi zinazoyanufaisha mataifa mengine, Mtafiti Kiongozi wa Programu ya Korosho Barani Afrika ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Profesa Peter Masawe, amesema kiasi kikubwa cha thamani ya korosho kinapotea kwa kukosa umakini. “Wabanguaji wa Tanzania wanachukua korosho karanga tu huku wakiacha kiasi kikubwa cha zao hilo ikiwemo maganda na mabibo ambayo yana thamani kubwa. Tutafute namna ya kuyaongezea thamani maganda na mabibo badala ya kutupa,” alisema. Profesa Masawe alitolea mfano mataifa yanayonufaika na korosho za Tanzania ikiwemo India: “Tujiulize kwa nini mataifa ya India, China na Vietnam ndio walionunu...

MAN U KUIVURUGA ENGLAND

Image
Manchester United wanajiandaa kutoa ofa ya kunasa saini ya winga wa Chelsea, Willian na beki wa Tottenham Toby Alderweireld, kwa mujibu wa taarifa kutoka ESPN. Jose Mourinho bado ni shabiki mkubwa wa Willian tangu walipokuwa wote pale Stamford Bridge ambapo Mbrazil huyo hajafurahishwa na kitendo cha kuwekwa benchi mara kwa mara na Antonio Conte msimu huu. Alderweireld, bado hajakubaliana na Spurs kuhusu mkataba mpya wa kubaki London na klabu yake inatarajiwa kumuuza ili kutunisha mfuko wa usajili majira ya kiangazi.

RAIS MAGUFULI KUKABIDHI KIKOMBE MSIMBAZI

Image
Uongozi wa shirikisho la soka Tanzania (TFF) kupitia Rais wake Wallace Karia, umetuma maombi kwa Waziri mwenye dhamana ya michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amuombe Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akabidhi kombe la VPL kwa Simba SC ambao ndiyo mabingwa wa msimu huu 2017/18. Simba itakabidhiwa kombe hilo siku ya Jumamosi Mei 19, 2018 baada ya mchezo wao wa mwisho wa ligi kwenye uwanja wa nyumbani (uwanja wa taifa) dhidi ya Kagera Sugar. Siku hiyohiyo pia Rais Magufuli atakabidhiwa kombe la CECAFA U17 Championship na timu ya vijana ya U17 ‘Serengeti Boys’ baada ya timu hiyo  kushinda kombe hilo Aprili 29, 2018 nchini Burundi. “Tumeandika barua kwa Waziri Mwakyembe amuombe ili Rais Magufuli akabidhiwe kombe la CECAFA U17 baada ya timu yetu kufanikiwa kushinda kombe hilo huko Burundi. Waziri amesema atajitahidi kwa kila njia ili Rais akubali.” “Pia kwa sababu siku hiyo Simba itakuwa inacheza mechi yake ya mwisho ya ligi kwenye uwanja wa nyumbani, tunafany...

MANARA KUACHANA NA CLUB YAKE

Image
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara amefunguka na kusema kwa sasa ameamua kuachana na klabu yake ya Manchester United hadi Kocha wa klabu hiyo Jose Mourinho atakapoondoka. Haji Manara amesema hayo siku moja baada ya klabu yake hiyo kupigwa bao 2 kwa moja na klabu ya Sevilla hivyo Manchester United kuondolewa kwenye mashindano ya klabu bingwa ulaya. "Guys kuna vitu siwezi kuviasi..1.Dini yangu,,2.wazazi wangu..Mke na watoto wangu na Simba...ila Manchester nimeiacha hadi Mourinho aondoke...Europe nimebaki na Madrid tu.....Kwangu Jose ndio mtu wa hovyo kupita wote duniani kwa sasa" alisema Haji Manara Siku tatu zilizopita wakati Manchester United ikikipiga na Liverpool aliahidi kama timu yake itafungwa angehama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuhamia CHAUMA lakini baahati nzuri timu yake ikashinda ila baada ya kupigwa na Sevilla ameamua kukaa pembeni mpaka kocha Jose Mourinho atakapoondoka.

WAMBURA AWEKWA KIKAANGONI TFF

Image
Kamati ya maadili ya TFF imekutana leo Machi 14, 2018 pamoja na mambo mengine kujadili suala la Makamu wa Rais wa Shirikisho hilo, Michael Wambura, aliyefikishwa kwenye kamati kwa makosa matatu.  Kwa mujibu wa Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo, amesema kuwa kosa la kwanza analokabiliwa nalo Wambura ni kupokea fedha za TFF. Pili, malipo yasiyo halali na tatu ni kugushi  barua na kushusha hadhi ya TFF.