Posts

Showing posts from September, 2017

MWANAHALISI WAICHIMBA MKWARA SERIKALI

Wamiliki wa gazeti la mwanahalisi lililofungiwa na serikali wamemtaka Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na michezo Anastazia Wambura kulifungulia gazeti hilo au watakutana mahakamani. Serikali imelifungia gazeti lao kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia Septemba 19 mwaka 2017. Waziri ametakiwa afungulie gazeti hilo ndani ya siku mbili kuanzia Jumatano vinginevyo watamfungulia mashtaka mahakamani. Licha ya kwenda Mahakamani Mwanahalisi itamdai fidia ya Shilingi milioni 41 yeye Naibu waziri binafsi kwa kila chapisho ambalo halitachapishwa kutokana na kufungiwa gazeti hilo. Kauli hiyo imetolewa Jumatano jijini Dar es salaam na mmoja wa wamiliki wa gazeti la Mwanahalisi Saed Kubenea katika mkutano wake na waandishi wa habari. Tayari mwanasheria wao amepeleka barua rasmi Jumanne kwa naibu waziri kwa vile amelifungia gazeti hilo wakati kuna amri ya Mahakama Kuu ya Dar es Salaam ya kutolifungia gazeti hilo. Hatua hii ni kuonyesha jinsi gani magazeti ya Mwanahalisi yanavyo sa...

MKUU WA WILAYA TUNDURU AZINDUA UPIGAJI CHAPA NG'OMBE

Image
Katika kutekeleza kwa vitendo sheria ya utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo namba 12 ya mwaka 2010 sambamba na kanuni zake za mwaka 2011 halmashauri ya wilaya ya Tunduru imefanya uzinduzi wa upigaji chapa ng’ombe mapema wiki hii katika Kijiji cha Muhuwesi ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Juma Zuberi Homera. Akisoma taarifa ya uzinduzi wa zoezi hilo la upigaji chapa ng’ombe,Afisa Mifugo na Uvuvi wilaya Dk Frank Mkoma alisema wilaya ya Tunduru ina jumla ya ng’ombe 62,685, mbuzi 5,974, kondoo 3,388 na nguruwe 2,650. Kati ya vijiji 157 vya wilaya ya tunduru ni vijiji 41 vilivyokwisha kufanyiwa matumizi bora ya ardhi na jumla ya hekta 11,480 zimetengwa kwa ajili ya malisho, eneo hili lina uwezo wa kulisha mifugo 11,480. Dk Mkoma alisema Halmashauri kwa awamu ya kwanza wanatarajia kupiga chapa ng’ombe wapatao 62,685 na watapigwa chapa kwenye mguu wa nyuma upande wa kulia. “Katika zoezi hili la upigaji chapa ng’ombe, wafugaji wote wa ngombe waliopo kwe...

UPINZANI KENYA KUFANYA MAANDAMANO KUPINGA TUME HURU YA UCHAGUZI (IEBC)

Image
Chama cha upinzani nchini Kenya NASA kimeitisha maandamano Jumanne nje ya makao makuu ya tume ya uchaguzi IEBC mjini Nairobi. Hatua hii ni ya kushinikiza kujiuzulu kwa baadhi ya maafisa wa juu wa tume hiyo walioshiriki kuandaa uchaguzi mkuu wa August 8 mwaka huu uliobatilishwa na mahakama ya juu nchini. NASA umeeleza kwamba hautovamia makao ya tume ya IEBC kama ilivyotajwa awali kuwatimua kwa lazima maafisa hao, badala yake unasema maandamano yatakuwa ya amani katika barabara za mji mkuu Nairobi kushinikiza kujiuzulu kwao. Hilo ni mojawapo ya masharti iliyotoa NASA kushiriki uchaguzi wa marudio uliotangazwa kufanyika Oktoba 26 mwaka huu. Rais Uhuru Kenyatta ametoa onyo kwa wapinzani ambao amesema watakumbana na mkono wa sheria iwapo maandamano yao yataingilia shughuli za kiuchumi za raia wa nchi hiyo. Im Amesema, 'Endeleeni na maandamano yenu, mukigusa mboga za mama wanaouza barabarani, tuko na nyinyi. Mukigusa maduka ya watu tuko na nyinyi. Lakini kama hamuna lingine...

MAREKANI YAANZA KUIHOFIA KOREA KASKAZINI

Image
Marekani imeilalamikia Korea Kaskazini, kwa kauli yake kuwa ina haki ya kuzitungua ndege za kivita za Marekani hata kama zipo nje ya anga la taifa hilo. Msemaji wa ikulu ya Marekani ya white house Sarah Huckabee Sanders, amewaambia waandishi wa habari kuwa kauli iliyotolewa na Waziri wa mambo ya kigeni wa Korea Kaskazini kwamba Marekani imetangaza vita,ni ya kipuuzi. Kauli hiyo ya waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini ni kufuatia ujumbe wa Rais Trump kupitia ukurasa wake wa twitter,uliokuwa ukisema utawala wa Pyongyoung hauwezi kudumu kwa muda mrefu. Akizungumza katika kituo cha mafunzo cha kimataifa mjini Washington,Waziri wa mambo ya nje wa Korea Kusini Kang Kyung-wha, amesema dunia inapaswa kupatiwa nafuu na maudhi ya Korea Kaskazini. "Hakika, hii inaonyesha kuwa Korea kaskazini itaendeleza maudhi yake, na katika mazingira kama haya,sisi Korea Kusini na umoja wa mataifa tunapaswa kulishughulikia suala hili kwa umakini mkubwa,ili kutoendeleza hofu ya madhara y...

TANGAZA BIASHARA YAKO NASI.

Image
TANGAZA BIASHARA YAKO,SHEREHE,MSIBA na SHUGHULI ZAKO ZOZOTE NASI KWA BEI NAFUU. #TUPIGIE +255 753394960 E–mail mkuwiahussein@gmail.com TANGAZA NASI ILI KUWAFIKIA WENGI ZAIDI.                            KARIBUNI SANA.

KENYA YAPOKWA KUANDAA MASHINDANO YA CHAN 2018

Kenya imepokonywa fursa ya kuandaa mashindano ya ubingwa wa Afrika wa mwaka 2018 (CHAN) kufuatia mkutanoa wa kamati kuu ya Caf uliofanyika Accra. Hatua hiyo ilitangazwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari baada ya mkutano wa siku moja uliioongozwa na rais wa Caf Ahmad. Caf inasema uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kuchelewa kwa ripoti za ukaguzi kadha uliofanywa nchini Kenya. Kinyanganyiro hicho ambacho kitashirikisha timu 16 kinatarajiwa kuanza tarehe 12 Januari hadi Februari mwaka 2018. Timu ya ukaguzi ya Caf ilizuru Kenya kuanzia tarehe 11 hadi 17 mwezi huu, na kupata kuwa ni uwanja mmoja tu kati ya viwanja vinne uliokuwa tayari kwa michuano hiyo. Shirikisho la kandanda nchini Kenya (FKF) linasisitiza kuwa lilifanya kila liwezalo kuhakikisha kuwa mashindano ya CHAN mwaka 2018 yangewezekana kwa Kenya na eneo lote la Afrika Mashariki.

WAZIRI MWAKYEMBE APIGA "STOP" MISS TANZANIA

Image
Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe amepiga marufuku mashindano ya Miss Tanzania na tuzo za muziki kutokana na ubabaishaji wa waandaaji wa mashindano ya tasnia hizo. Mwakyembe amesema mashindano ya Miss Tanzania yamegubikwa na ubabaishaji kwenye utoaji wa tuzo na kumekuwa na tabia ya kuchelewa kuwapa washindi zawadi wanazoahidiwa jambo linaloleta usumbufu. Waziri huyo ameongeza kuwa watakaotaka kuandaa mashindano hayo ni lazima zawadi wanazoahidi kuwapa washindi zipekwe ofisini kwake. ”Kwa sasa tunanakaa chini na wadau wa burudani juu ya mashindano hayo ila tunataka tuzo ziwe na (guaranteed sustainability) muendelezo wa uhakika na sio kufanyika kwa kubahatisha”, alisema Mwakyembe. Kwa mara ya mwisho mashindano ya za Miss Tanzania yalifanyika mwaka 2016 ambapo ilichukua takribani miezi 6 kwa Kamati ya shindano la Urembo la Miss Tanzania kumpatia mshindi zawadi yake. Gari aina ya (Suzuki Swift) aliloshinda Miss Tanzania 2016 Diana Edward baada ya miezi 6 m...

MWALIMU MBARONI KWA KUMJAZA MIMBA MWANAFUNZI

Image
Mwalimu wa shule ya msingi Samazi iliyoko Wilayani Kalambo mkoani Rukwa, anashikiliwa na polisi wa mkoa huo kwa tuhuma za kumbaka na kisha kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la sita, mwenye umri wa miaka 15.   Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Judith Binyura amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi baada ya mwanafunzi huyo (jina limehifadhiwa) kumtaja kwamba ndiye aliyempa ujauzito huo.   "Tumekuwa na utaratibu kuwapima mimba watoto wa shule ili kubaini kama wana ujauzito,  sasa safari hii katika shule ya Samazi imegundulika kuwa mwanafunzi wa darasa la sita amepewa ujauzito na mwalimu wake," amesema .   Mratibu Elimu Kata ya Samazi, Daudi Sengo amesema mwalimu huyo alikuwa akimtuma mwanafunzi huyo kufanya kazi za nyumbani kwake kama kufua, kusafisha nyumba na kumpikia chakula cha jioni na kisha kufanya naye mapenzi mara kwa mara.   Ameongeza awali ilikuwa vigumu kuthibitisha kuhusu uhusiano wao wa kimapenzi hadi mwanafunzi huyo alipopimwa na kubainika ni mjamzit...

MAAFISA WA TUME YA UCHAGUZI NA MIPAKA KENYA (IEBC) MATATANI

Image
Upinzani nchini Kenya Nasa umempatia mkurugenzi wa mashtaka nchini humo Keriako Tobiko saa 72 kuwafungulia mashtaka maafisa wa IEBC wanaotuhumiwa kuharibu uchaguzi wa Agosti 8. Wakati huohuo upinzani huo umeapa kuwafungulia mashtaka ya kibinafsi maafisa hao wa IEBC. Nasa imesema kuwa mahakama ya juu siku ya Jumatano haikuwaondolea lawama maafisa wa IEBC na kwamba ni sharti washtakiwe kwa kufanya udanganyifu katika uchaguzi huo. ''Kufuatia uamuzi uliotolewa na mahakama ya juu, afisi yako imesema kwamba inaangazia uamuzi huo kwa kina na kufanya uamuzi wa iwapo itawafungulia mashtaka ya uhalifu maafisa wa IEBC au la.Uelewa wetu ni kwamba makamishna na wafanyikazi wakuu wa IEBC walitekeleza uhalifu'', alisema Mbunge Mathare MP Anthony Olouch. Aliongezea: Kutokana na uchaguzi wa marudio uliotangzwa kufanyika tarehe 26, kctoba 2017, maafisa waliorodheshwa hapa chini hawataruhusiwa kusalia afisini ili kuendeleza uhalifu waliotekeleza. Image caption Mwenyekiti wa tume...

LORI LA DANGOTE LAKAMATWA NA WAHAMIAJI HARAMU

Image
Dar es Salaam. Wahamiaji haramu wanane kutoka Ethiopia wamekamatwa wakisafirishwa kwa lori la kampuni ya Dangote kwenda Mtwara. Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Edward Chegero amesema leo Alhamisi kuwa, wahamiaji hao walikamatwa Kongowe wilayani Temeke. Amesema wamekamatwa jana Jumatano baada ya idara kupata taarifa na baadaye kuweka mtego uliowanasa. Chegero amesema mbali na wahamiaji hao, idara imewakamata Watanzania wanne waliokuwa wakiwasindikiza wahamiaji hao. Amesema Watanzania hao walikuwa wakitumia gari aina ya Toyota Passo. Kaimu kamishna amesema uchunguzi unaendelea ili kuwakamata wahusika wote wa mtandao huo. Chegero amesema baadhi ya wahamiaji hao walikuwa na tiketi zinazoonyesha wanatoka Msata kwenda Dar es Salaam. Amewataka madereva wa malori na usafiri mwingine kutosafirisha wahamiaji haramu kwa kuwa kufanya hivyo ni kuvunja cha sheria. Kaimu kamishna pia amewaonya wamiliki wa nyumba za wageni zinazotumika kuwaficha wahamiaji hao akisema ki...

NYALANDU KUMPELEKA LISSU MAREKANI

Image
Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ameweka kambi nchini Kenya kuangalia uwezokano wa kupata ruhusa kutoka kwa   madaktari ya kumsafirisha Mh Tundu Lissu kwenda Marekani kwaajili ya matibabu zaidi baada kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana. Nyalandu amedai ni siku ya tatu bado hajapata ripoti inayoonyesha maendeleo ya mgonjwa huyo ili waangalie kama wanaweza kwenda nchini Marekani kwaajili ya matibabu zaidi. ==> Hii  ni Taarifa ya Mh Nyalandu 

GAZETI LA MWAHALISI LAPIGWA KUFULI

Image
Serikali ya Tanzania imelifungia gazeti la Mwanahalisi kwa miaka miwili zuio hilo pia linahusisha machapisho ya mtandaoni . Gazeti hilo linafungiwa kwa kile kilicho arifiwa kuwa ni kuchapisha habari za uongo na uchochezi ambazo zinadaiwa kuwa zinaweza kuhatarisha usalama wa taifa. Mwanahalisi linakuwa gazeti la pili kufungiwa kwa kipindi cha miezi minne . Gazeti hilo limepigwa kufuli kutokana na kuchapisha mlolongo wa habari ambazo zinasemekana kuwa za kichochezi ikiwemo yenye kichwa cha habari 'Tumwombee Magufuli au Tundu Lissu' iliyochapishwa katika toleo la 409 la tarehe 18-24 Septemba 2017 . Hivi karibuni vyombo vya habari vimekuwa vikimulikwa kwa ukaribu nchini humo. Mapema mwaka huu Raisi Magufuli alionya vyombo vya habari 'visifikiri viko huru kwa kiwango hicho.'

ZITTO AFUNGUKA KUHUSU TUNDU LISSU

Image
NA HUSSEIN MKUWIA Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amefunguka na kudai amerudi nchini akiwa na unyenyekevu mkubwa zaidi kwa sababu ya nguvu na ujasiri alionyeshwa na Mbunge Tundu Lissu pindi alipokwenda kumjulia hali katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya . Zitto ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa facebook na kusema japo Lissu ameumizwa sana lakini hakuacha kumuonyesha ucheshi licha ya kuwa na maumivu makali aliyokuwa nayo katika mwili wake. "Siku mbili hizi nilizomuona Lissu kitandani zimeniacha nikifikiria sana, nimerudi nchini nikiwa kwenye unyenyekevu zaidi kwa sababu ya nguvu na ujasiri ambao ndugu yangu amenionyesha licha ya kuwa kwenye maumivu makali. Siyo mara nyingi hapa nchini utasikia tukiongelea ujasiri lakini namfikiria lissu na vile nilivyojisikia nikiwa pamoja naye Nairobi, najua hivyo ndivyo alivyo",  ameandika Zitto. Zitto ameendelea kwa kusema  "waliomshambulia wamemuumiza kweli na bado wakati t...

JESHI LA KOREA KASKZINI KUFANANA NA MAREKANI

Image
Korea Kaskazini imetangaza kuwa lengo lake kuu kijeshi kwa sasa ni kuhakikisha inakuwa na uwezo sawa na Marekani . Shirika la habari la Korea Kaskazini lilitoa taarifa hiyo baada ya kombora la majaribio la mwisho kufanywa, ikisema kuwa kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong-Un, amesema kuwa hataki kusikia Marekani ikisema itakabiliana na Korea Kaskazini kijeshi. KIongozi wa taifa hilo Kim Jong un ameapa kuhakikisha kuwa taifa hilo linaafikia mpango wake wa kinyuklia kulingana na vyombo vya habari vya taifa hilo. Lengo lake ni kuhakikisha jeshi la tifa hilo lina uwezo sawa na lile la Marekani kulingana na chom,bo cha habari cha KCNA kilichomnukuu kiongozi huyo. Haki miliki ya picha Image cap Matamshi ya bwana Kim yanajiri baada ya taifa hilo kufanyia majaribio kombora lake kupitia anga ya Japan, likitajwa kuwa kombora lililosafiri kwa umabli mkubwa zaidi .Hatua hiyo imesbabishwa mgawanyiko miongoni mwa mataifa ambayo yaliunga nyuma ya uMoja wa Matifa dhidi ya Korea kaskazini siku...

WATU WAWILI WAUWAWA TUNDURU

Na Hussein Mkuwia. Watu wawili wamefariki dunia katika majibizano ya risasi kati ya polisi na watu hao katika kijiji cha Nangunguru, kata ya Nandembo Tarafa ya Nampungu Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma  Watu wawili wamefariki dunia katika majibizano ya risasi kati ya polisi na watu hao katika kijiji cha Nangunguru, kata ya Nandembo Tarafa ya Nampungu Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Gemini Mushi, polisi hao wakiwa katika majukumu mbalimbali ya ulinzi wa raia na mali zao katika kijiji cha Nangurukuru walikutana na watu wakiwa kwenye pikipiki walijaribu kuwasimamisha walikaidi amri na kuanza kurusha risasi. Kamanda Mushi amesema kuwa polisi kwa kutumia mbinu za medani walifanikiwa kuwashinda watu na hao na kuwapiga risasi na kufa papo hapo, ambapo walikutwa na bunduki aina SR pamoja na risasi 41 zinazotumiaka na silaha h Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Gemini Mushi, polisi hao wakiwa katika majukumu mbalimbali ya ulinz...