VINARA wa Ligi Kuu Tanzania bara, Simba wanatarajiwa kuendeleza rekodi yao ya kufanya vizuri bila kupoteza katika mchezo dhidi ya Mbao FC utakaochezwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Simba inajivunia kwa kila kitu. Inaongoza kileleni kwa pointi 23 katika michezo tisa iliyocheza kati ya hiyo imeshinda saba, imepata sare mbili, ikiwa na jumla ya mabao ya kufunga 17 na kuruhusu kufungwa matatu pekee. Timu hiyo inajivunia mchezaji wake Shizza Kichuya akiongoza katika safu ya ushambuliaji kwa kufunga mabao saba peke yake hadi sasa, huku wengine katika timu nyingine wakifunga kuanzia manne. Hiyo ni kabla ya matokeo ya jana. Iwapo itaendeleza ushindi itajiwekea rekodi ya kucheza michezo 10 bila kupoteza. Lakini pia, macho yataendelea kuwatazama washambuliaji wake wenye uchu wa kufunga wakati wote ambao ni Kichuya, Ibrahim Ajib na Laudit Mavugo. Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja alisema kuwa ikiwa kikosi chake kitaendeleza umoja ilionao sasa, basi njia itakuwa nyeup...
SERIKALI imo katika mchakato wa kuanzisha kiwanda cha korosho Mkuranga, Mtwara na Tunduru katika mwendelezo wa juhudi za kuwa na Tanzania ya uchumi wa kati na ya viwanda. Tanzania inazalisha tani 260,000 za korosho kwa mwaka na sasa ina viwanda 12 vya ubanguaji. Akizungumza Dar es Salaam jana juu ya umuhimu wa kuacha utaratibu wa kusafirisha korosho ghafi zinazoyanufaisha mataifa mengine, Mtafiti Kiongozi wa Programu ya Korosho Barani Afrika ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Profesa Peter Masawe, amesema kiasi kikubwa cha thamani ya korosho kinapotea kwa kukosa umakini. “Wabanguaji wa Tanzania wanachukua korosho karanga tu huku wakiacha kiasi kikubwa cha zao hilo ikiwemo maganda na mabibo ambayo yana thamani kubwa. Tutafute namna ya kuyaongezea thamani maganda na mabibo badala ya kutupa,” alisema. Profesa Masawe alitolea mfano mataifa yanayonufaika na korosho za Tanzania ikiwemo India: “Tujiulize kwa nini mataifa ya India, China na Vietnam ndio walionunu...
Comments
Post a Comment