DC TUNDURU AHAIDI KUWASOMESHA WATOTO WANNE

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera(kushoto) akizungumza na watoto alioahidi kuwasomesha
  NA HUSSEIN MKUWIA

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mkoani Ruvuma Juma Homera ameahidi kuwasomesha wanafunzi wanne zikiwa ni juhudi za serikali kuhamasisha wazazi kupeleka watoto wao shule hasa awamu hii ambapo serikali ya awamu ya tano inatoa elimu Bure.

Waliyopata bahati hiyo adhimu kutoka kwa mkuu wa Wilaya huyo ni wanafunzi waliohaguliwa kujiunga na masomo ya Sekondari mwaka wa masomo 2017 kutoka katika kijiji cha Nambalapi Kata ya Masonya wilayani humo.

Homera alitoa ahadi hiyo wakati akiongea na wananchi wa Kijiji hicho katika mkutano wa kuhamasisha shughuli za maendeleo katika kata hiyo uliofanyika katika viwanja vya ofisi za kijiji hicho.

Homera amewataja wanafunzi hao kuwa ni  Somoye Bakari,Awetu Ally,Amina Rajab na Sada Hamisi ambaye ni yatima.

Comments

Popular posts from this blog

SIMBA SC YATAMBA KUENDELEZA REKODI YAO LEO

SINEMA YA CUF NA PROF LIPUMBA YAFIKIA PATAMU