WAFUGAJI WAUA MKULIMA

Tokeo la picha la ZUBERI MUHOMBEJI

NA HUSSEIN MKUWIA

POLISI Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma inawasaka  wafugaji jamii ya Kimang’ati ili kujibu tuhuma ya mauaji ya mkulima katika kijiji cha Lukala tarafa ya Lukumbule. 

Katika taarifa hiyo, Kamanda Muhombeji  alimtaja mtu aliyekumbwa na mkasa huo kuwa ni Issa Kasimu Issa  (27) na kwamba mkasa huo ulimpata wakati akiwa katika mazizi ya wafugaji hao nje kidogo ya kijijini hicho.

Tukio hilo lilitokea Januari  7, 2017 katika kijiji cha Lukala pembezoni mwa mto Ruvuma,  eneo ambalo walikuwa wakiishi wafugaji hao wanaodaiwa kuwa na urafiki  wa muda mrefu na marehemu, na kwamba walikuwa wakimpatia ng’ombe na kwenda kuwauzia na kuwapelekea fedha.
 
Hivyo jeshi la polisi mkoani ruvuma limewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zenye usahihi zitakazowezesha watuhumiwa kukamatwa ili sheria iweze kufuata mkondo wake.



Comments

Popular posts from this blog

SIMBA SC YATAMBA KUENDELEZA REKODI YAO LEO

SINEMA YA CUF NA PROF LIPUMBA YAFIKIA PATAMU