Posts

Showing posts from October, 2016

THOMAS MASHALI AFARIKI DUNIA

Image
Bondia nguli wa ngumi za kulipwa nchini Thomas Mashali maarufu kama Simba asiyefugika amefariki dunia usiku wa kuamkia leo juma tatu october 31,2016 kwa kushambuliwa na watu wasiojulikana maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam. Inaelezwa kuwa, Mashali alishambuliwa na watu wasiojulikana na kumuita mwizi, mwili wake uliokotwa vichakani huko maeneo ya Kimara na kufikishwa hospitali ya muhimbili na ndipo umauti ulipomkuta. Taarifa zaidi zitakujia kadiri zitakavyotufikia

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OCTOBER 22, 2016

Image

LIGI DARAJA LA KWANZA KUENDELEA LEO

Image
Wakati mzunguko wa tano wa Ligi Daraja la Kwanza ukitarajiwa kuendelea kesho Jumamosi na keshokutwa Jumapili, Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeagiza makamishna na wakuu wa vituo kuzuia wachezaji wote ambao hawana leseni kutocheza. Hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14 (16), inayosema: “Wachezaji wote watatambulika kwa kutumia leseni zao zitakazotolewa na kuidhinishwa na TFF. Mchezaji yoyote ambaye hatakuwa na leseni hataruhusiwa kucheza katika mchezo husika.”  Kipindi cha dharura amvacho TFF ilikitoa ni kwa mizunguko mitatu ya mwanzo, lakini taarifa za makamishna zinaonyeha kuwa raundi ya nne bado kuna timu zilikuwa zinatumikia leseni za muda ilihali walikwisha kutaarifiwa kuwa leseni zao ziko tayari na wao wanakwama kuzifuata hapa TFF. Kuanzia sasa hakuna sababu yoyote itakayotolewa na ikaeleweka kwa mchezaji ambaye hatakuwa na leseni.  Kwa mujibu wa ratiba ya Ligi Daraja la Kwanza, michezo ya Kundi A kesho itakuwa ni kati ya Pamba y...

LEO JUMAMOSI OCTOBER 22, 2016. RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND, HISPANIA, UJERUMANI NA ITALIA.

Image

VIWANJA SITA KUTIBUKA VUMBI LEO JUMAMOSI VPL, VIWILI KESHO JUMAPILI.

Image
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu 2016/17, raundi ya 12 inaendelea leo kwa michezo sita kupigwa ambapo mabingwa watetezi Young Africans ya Dar es Salaam itakuwa mgeni wa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba ulioko Bukoba mkoani Kagera. Jijini Dar es Salaam, katika Uwanja wa Uhuru African Lyon itakuwa mwenyeji wa Mbeya City ya Mbeya ilhali Mwadui ya Shinyanga itasafiri hadi Mtwara kucheza na Ndanda Fc kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona wakati Stand United itakuwa mgeni wa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye mchezo utaofanyika Uwanja wa Manungu, ulioko Turiani – Mvomero. Majimaji itakuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja wa Majimaji huko Songea. Mchezo kati ya Azam FC na JKT Ruvu utaanza saa 1.00 usiku kwenye Uwanja wa Azam Chamazi-Mbagala Dar es Salaam. Na kesho Jumapili itakuwa ni zamu ya kinara wa ligi hiyo, Simba ambayo itaikaribisha Toto Africans ya Mwanza kwenye Uwanja wa Uhuru wakati Tanzania Prisons itapambana na Mbao FC kwenye Uwanja wa Kumbuku...

"YANGA SIO MASUFURIA YA SHUGHULI"

Image
Ikiwa yamesalia masaa machache kabla ya kufanyika kwa mkutano mkuu wa dharura wa klabu ya Yanga, Katibu wa baraza Wazee wa Yanga Ibrahim Akilimali amesema yeye pamoja na wanachama wengine hawakubaliani na mchakato wa Manji kuikodi klabu ya Yanga. Akilimali amehoji lilipotoka deni la zidi ya shilingi bilioni 11 kitu ambacho kimewastusha sana wanachama. Wakati huohuo ikaibuka hoja kwamba Mwenyekiti wa klabu hiyo akodishwe Yanga na neno yake kwa miaka 10. “Yanga ni klabu kubwa sana yenye historia kubwa, haiwezi ikakodishwa sawa na masurufia ya shuhulini”, amesema Mzee Akilimali. Akilimali amezidi kusema kwamba, Manji angefata utaratibu ili kuwapa nafasi wanachama ya kupatiwa elimu ya faida na hasara ya jambo hilo kabla ya kuwaita wanachama ili wakubali au wakatae mchakato huo kabla ya kutia saini au kutotia saini mkataba huo wa kuthibitisha kukodishwa kwa klabu ya Yanga.

STAND FC YAANZA KIBABE HASSAN MUYAO CUP

Image
Mashindano ya kombe la HASSAN MUYAO yameanza kutimua vumbi leo ijumaa october 21,2016 katika kiwanja cha ccm wilayani Tunduru kwa kuzikutanisha Stand FC dhidi ya Chapate FC yenye makao yake mtaa wa Ausilinda. Mchezo huo ambao ulianza kwa timu zote mbili kushambuliana kwa kasi na zikicheza kwa umakini wa hali ya juu na kutoruhusu kutikiswa chavu za lango la kila timu mpaka kumalizika kwa kipindi cha kwanza Stand  FC 0-0 Chapate FC. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na taadhari ya aina yake kwa kila timu, lakini Chapate FC walionekana kuzidiwa na kuruhusu mashambulizi langoni mwao. Ndipo washambuliaji wa Stand FC wakatumia udhaifu wa safu ya ulinzi ya Chapate FC na kuanza kufungua ukurasa wa magoli dakika ya 55 na 70 yakifungwa na Ballotel, Razack dakika ya 63, huku na Shaibu akafunga ukurasa huo wa magoli dakika ya 82. Huku  goli pekee la kufutia machozi la Chapate FC likiwekwa kimiani na mshambuliaji wa Rashidi dakika za lala kwa buriani 90 na kufanya mbao ya matoke...

UJENZI WA NYUMBA BUKOBA NI TSH 880 BILIONI

Image
SERIKALI mkoani Kagera imesema  tathimini iliyofanyika  ya athari za tetemeko la ardhi mkoani hapo imebaini ujenzi wa makazi ya watu kurejea kwenye hali yake kunahitaji   Sh bilioni 880  huku ujenzi wa miundombinu  ya serikali ukihitaji Sh bilioni  tisa. Mkuu wa Mkoa Kagera, Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, aliyasema wakati akipokea msaada wa fedha  na vitu mbalimbali yakiwamo  mablanketi  na vyandarua kutoka kwa taasisi ya Adra Tanzania ya Kanisa  la Adventisti Tanzania lenye makao makuu yake  Arusha. Kijuu alisema hadi sasa fedha zilizoingizwa katika akaunti ya maafa ya Kagera ni   Sh bilioni nne  ambazo hazitoshelezi katika ujenzi wa makazi ya watu. Alisema   serikali  imependekeza  vifaa vingine vipelekwe katika taasisi za umma vikiwamo vituo vya afya na  shule  wananchi waendelee kupata huduma kama ilivyokuwa  awali.

MBARONI KWA KUJIFANYA MWANASHERIA

Image
JESHI la polisi mkoani Mara, linamshikilia mtu mmoja aliyejifanya mwanasheria wa kujitegemea. Mtu huyo alidaiwa  kufanya utapeli wa mamilioni ya shilingi kwa watu mbalimbali aliowafuata   kuwasaidia katika  masuala ya sheria. Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Ramadhani Ng’anzi,alisema mtu huyo,   Joel Robert,alikamatwa Oktoba 13 katika Kijiji cha Kiterere wilayani Tarime baada ya   kumfuatilia. Alisema mtu huyo alikuwa amekwisha kuwatapeli watu wengi ambao majina yao yanahifadhiwa. Kamanda alisema mtu huyo  amekuwa akiwatapeli watu kwa nyakati tofauti akijifanya ni wakili wa kujitegemea na kufuatilia masuala ya kesi kwenye vituo vya polisi na mahakama. Ng’anzi alisema baada ya kupata taarifa za mtu huyo waliwatumia maaofisa wa upelelezi kumfuatilia na kumkamata na hivi sasa anaendelea kuhojiwa kabla ya kufikishwa mahakamani. “Mtu huyu amefanya utapeli kwa muda mrefu kutokana na taarifa za watu waliotapeliwa ambao waliz...

MATOKEO YA MECHI ZOTE ZA EUROPA LEAGUE ZILIZOCHEZWA ALHAMISI OCTOBER 20, 2016

Image

GENK YA SAMATA YAPAA KILELENI KUNDI F LIGI YA EUROPA

Image
Usiku wa October 20 imepigwa michezo ya UEFA Europa League, lakini kwa upande wa watanzania wao walikuwa wakisubiri kumshuhudia mshambuliaji wao wa kimataifa Mbwana Samatta akiiwakilisha klabu yake ya Genk kwenye michuano hiyo ya Ulaya. Katika mchezo huo ambao Genk iliibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Atletico Bilbao na kukusanya pointi tatu wakiutumia vyema uwanja wao wa nyumbani Cristal Arena, Samatta aliingia dakika ya 56 kipindi cha kuchukua nafasi ya Thomas Buffel. Magoli ya Genk yamefungwa na Jakub Brabec aliyefungua nyavu za Bilbao dakika tano kabla ya kwenda mapumziko huku zikiwa zimesalia dakika mbili pambano kumalizika, mnigeria Onyinye Wilfred Ndidi akafunga bao la pili na la ushindi kwa Genk. Genk inaongoza Kundi F ikiwa na pointi 6 baada ya kucheza mechi tatu hadi sasa. Katika mechi zake tatu, imeshinda mbili na kupoteza mechi moja, imefanikiwa kufunga magoli 7 huku yenyewe ikiwa imeruhusu magoli manne hivyo kufanya tofauti ya magoli ya kufun...

KICHUYA APA DILI AFRIKA KUSINI

Image
Baada ya kuonyesha kiwango cha juu tangu atue klabu ya Simba winga Shiza Kichuya huenda akaihama timu hiyo na kutua Chippa United ya Afrika Kusini baada ya benchi la ufundi la timu hiyo kuvutiwa naye. Wakala wa kusaka wachezaji wa Chippa, Rodgers Mathaba ameiambia blog ya  blacknationtz , kuwa wamevutiwa na mchezaji huyo baada ya kumfatilia katika baadhi ya mechi alizoichezea timu yake ya Simba na anatarajia kutua nchini hivi karibuni kwa ajili ya kufanya mazungumzo na uongozi wa timu hiyo. “Tumevutiwa na kipaji cha Kichuya na tupo tayari kumnunua endapo tutafikia muafaka na klabu yake anayoichezea ya Simba sc,” amesema Mathaba.  Hiyo itakuwa ni neema kwa Simba na Kichuya mwenyewe ambaye ametua Simba msimu huu akitokea Mtibwa Sugar ya mkoani morogoro na amekuwa na mwanzo mzuri hadi kufikia hapo alipo.

SIMBA SC YATAMBA KUENDELEZA REKODI YAO LEO

Image
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania bara, Simba wanatarajiwa kuendeleza rekodi yao ya kufanya vizuri bila kupoteza katika mchezo dhidi ya Mbao FC utakaochezwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Simba inajivunia kwa kila kitu. Inaongoza kileleni kwa pointi 23 katika michezo tisa iliyocheza kati ya hiyo imeshinda saba, imepata sare mbili, ikiwa na jumla ya mabao ya kufunga 17 na kuruhusu kufungwa matatu pekee. Timu hiyo inajivunia mchezaji wake Shizza Kichuya akiongoza katika safu ya ushambuliaji kwa kufunga mabao saba peke yake hadi sasa, huku wengine katika timu nyingine wakifunga kuanzia manne. Hiyo ni kabla ya matokeo ya jana. Iwapo itaendeleza ushindi itajiwekea rekodi ya kucheza michezo 10 bila kupoteza. Lakini pia, macho yataendelea kuwatazama washambuliaji wake wenye uchu wa kufunga wakati wote ambao ni Kichuya, Ibrahim Ajib na Laudit Mavugo. Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja alisema kuwa ikiwa kikosi chake kitaendeleza umoja ilionao sasa, basi njia itakuwa nyeup...

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA ATUMBULIWA

Image

EDDO AIPA SIMBA UBINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA

Image
Mchambuzi wa masuala ya soka nchini Eddo Kumwembe ametoa tathmini yake juu ya mwendelezo mzuri wa matokeo inayopata klabu ya Simba katika mechi zake za ligi kuu Tanzania bara (VPL) tangu kuanza kwa msimu huu ikiwa bado haijapoteza mchezo katika mechi zake 9 ilizocheza hadi sasa. Eddo amesema ‘Wekundu wa Msimbazi’ wapo kwenye nafasi mzuri ya kutwaa taji la VPL msimu huu baada ya misimu minne mfululizo kupita wakishuhudia taji hilo lienda kwa mahasimu wao Jangwani na kwa matajiri wa dar Azam fc (Chamazi). “Kwa mtazamo wangu nadhani Simba wapo kwenye nafasi nzuri ya kuchukua ubingwa kwasababu wamesajili wachezaji wazuri. Ukiangalia wachezaji wengi wanaoisaidia Simba kwa sasa ni wachezaji wapya, kwahiyo inaonesha kwamba wamefanya usajili mzuri,” amesema Eddo alipokua akitoa maoni yake kwenye kituo cha radio juu ya mwendelezo mzuri wa matokeo ya klabu ya Simba “Ukiangalia mlinzi wao wa kulia (Boukungu), Mzamiru, Kichuya, Mwanjale ni wachezaji wapya walioingia kwenye kikosi cha kwan...

KICHUYA MCHEZAJI BORA LIGI KUU TANZANIA BARA MWEZI SEPTEMBA

Image
Shirikisho la soka nchini TFF limemtangaza mshambuliaji wa klabu ya Simba Shiza Kichuya kuwa mchezaji bora wa mwezi September baada ya jopo la wataalamu kuchambua kwa kina na kuona mchezaji huyo amekidhi vigezo vya kuwa mshindi wa tuzo hiyo  akiwabwaga wachezaji wengine wawili. Alfred Lucas amemtangaza Kichuya kushinda tuzo hiyo akifuata nyayo za John Boco aliyeshinda tuzo hiyo kwa mwezi August. “Mshambuliaji wa Simba Shiza Ramadhani Kuchua amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi September.” “Kichuya amewashinda washambuliaji Adam Kingwande wa Stand United na Omary Mponda wa Ndanda FC.” “Kichuya aliisaidia klabu yake ya Simba katika mwezi September kupata pointi 12 katika mechi nne ambazo ilicheza matokeo ambayo yameifanya Simba kuendelea kuongoza ligi.” “Alifunga mabao matatu katika mechi mbili kati ya nne alizocheza. kwa kushinda tuzo hiyo ya mwezi, Kichuya atazawadiwa kiasi cha shilingi milioni moja kutoka kwa mdhammini wa ligi kuu Tanzania bara.”

MKEMI: "YANGA HAIKODISHWI"

Image
Siku chache baada ya agenda za mkutano mkuu wa dharura wa Yanga kuwekwa hadharani, mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo aliyefutwa uanachama katika mkutano wa dharura uliopita Salum Mkemi amepinga mkutano huo ulioitishwa na Mwenyekiti wa Yanga Yusuf Manji ukitarajiwa kufanyika October 23. Mkemi amesema mkutano huo wa dhrula si halali huku pia akipinga mpango wa timu hiyo kukodishwa kwamba ni kinyume na utaratibu huku akisisitiza kwamba yeye bado ni mwanachama na mjumbe halali wa klabu ya Yanga . “Mimi bado mjumbe wa kamati ya utendaji, sheria na katiba yangu ndivyo inavyosema, Manji kachaguliwa kama nilivyochaguliwa mimi. Kama vile Magufuli alivyochaguliwa, Rais hawezi kusitisha kazi ya mbunge kwasababu yeye si aliyemchagua. Mbunge amechaguliwa na wananchi, mbunge wa kuteuliwa ndio anaweza akamuondoa, mimi nimepigiwa kura kama Manji alivyopigiwa kura.” “Huo upuuzi wake anaotaka kuufanya Jumapili utamtokea puani, Yanga wenyewe tupo hatujafa na hatujalala. Yanga haikodishw...

SAMATTA, WANYAMA KUSHINDANIA TUZO YA CAF

Image
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayechezea soka ya kulipwa Ubelgiji Mbwana Ally Samatta ni miongoni mwa wachezaji 30 walioteuliwa kushindania Tuzo ya shirikisho la soka barani Afrika (CAF) ya Mchezaji Bora wa Afrika. Mkenya Victor Wanyama ambaye kwa sasa anachezea klabu ya Tottenham pia ameteuliwa.     Samatta asaidia klabu yake kufuzu Europa League Kutoka DR Congo kuna Yannick Bolasie anayechezea Everton.     Pochettino: Mkenya Wanyama ni ‘mnyama’ Orodha kamili hii hapa: 1. Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City) 2. El Arabi Hillel Soudani (Algeria & Dinamo Zagreb) 3. Islam Slimani (Algeria & Leicester City) 4. Samuel Eto'o (Cameroon & Antalyaspor) 5. Benjamin Mounkandjo (Cameroon & Lorient) 6. Serge Aurier (Cote d'Ivoire & PSG) 7. Eric Bailly (Cote d'Ivoire & Manchester United) 8. Yao Kouasi Gervais 'Gervinho' (Cote d'Ivoire & Hebei Fortune) 9. Mohamed Salah (Egypt & Roma) ...