YANGA YAZIBURUZA AZAM NA SIMBA VIWANGO VYA CAF
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa viwango vya ubora wa klabu barani, huku Yanga ikiongoza kwa klabu za Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Yanga SC imeshika nafasi ya 331 mbele ya Azam FC iliyo katika nafasi ya 351, wakati klabu nyingine ya Tanzania iliyoingia ni Simba SC iliyo katika nafasi ya 356.
Esperance ndiyo inaongoza kwa ubora wa soka Afrika, ikifuatiwa na Etoile du Sahel, zote za Tunisia, TP Mazembe, AS Vita zote za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), El Merreikh ya Sudan, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, Al Ahly ya Misri, Al Hilal ya Sudan, Zamalek ya Misri na Coton Sport ya Cameroon katika 10 Bora.
Comments
Post a Comment