UJENZI WA NYUMBA BUKOBA NI TSH 880 BILIONI


SERIKALI mkoani Kagera imesema  tathimini iliyofanyika  ya athari za tetemeko la ardhi mkoani hapo imebaini ujenzi wa makazi ya watu kurejea kwenye hali yake kunahitaji   Sh bilioni 880  huku ujenzi wa miundombinu  ya serikali ukihitaji Sh bilioni  tisa.

Mkuu wa Mkoa Kagera, Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, aliyasema wakati akipokea msaada wa fedha  na vitu mbalimbali yakiwamo  mablanketi  na vyandarua kutoka kwa taasisi ya Adra Tanzania ya Kanisa  la Adventisti Tanzania lenye makao makuu yake  Arusha.

Kijuu alisema hadi sasa fedha zilizoingizwa katika akaunti ya maafa ya Kagera ni   Sh bilioni nne  ambazo hazitoshelezi katika ujenzi wa makazi ya watu.

Alisema   serikali  imependekeza  vifaa vingine vipelekwe katika taasisi za umma vikiwamo vituo vya afya na  shule  wananchi waendelee kupata huduma kama ilivyokuwa  awali.

Comments

Popular posts from this blog

SIMBA SC YATAMBA KUENDELEZA REKODI YAO LEO

AZAM FC,SIMBA SC ZAFANYA KUFURU USAJILI DIRISHA DOGO