Popular posts from this blog
UWANJA WA TAIFA KUFUNGWA CAMERA ZA ULINZI (CCTV)
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametimiza ahadi yake ya ufungwaji wa kamera za ulinzi (CCTV) kwenye uwanja wa Taifa na kuhimiza zianze kutumika kwenye mechi mbalimbali ili kuwabaini waharibifu wa miundombinu. Nape alitoa agizo hilo jana alipotembelea kukagua viti vilivyovunjwa na mashabiki wa Simba katika mechi yake dhidi ya Yanga Oktoba mwaka huu na kukagua ufanisi wa kamera 119 za kufuatilia matukio yote uwanjani. Alisema kazi ya kubaini waharibifu wa miundombinu kwa sura katika uwanja huo kwa kutumia kamera hizo utasaidia kuongeza hali ya usalama kwenye uwanja na pia kusaidia kufuatilia matukio ya kihalifu uwanjani kama vile kuvunja viti. “Kwa sasa uwanja wetu utaweza kushughulika na mtu mmoja mmoja anayehujumu miundombinu yetu, kwa sababu kamera zetu zina uwezo mkubwa wa kumtambua mtu kwa sura pindi awapo uwanjani kuanzia magetini,” alisema. Ufungwaji wa kamera hizo ni ahadi ya Waziri Nape aliyowahi kuitoa baada ya mashabiki wa Simba na Yanga...
SIMBA SC YATAMBA KUENDELEZA REKODI YAO LEO
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania bara, Simba wanatarajiwa kuendeleza rekodi yao ya kufanya vizuri bila kupoteza katika mchezo dhidi ya Mbao FC utakaochezwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Simba inajivunia kwa kila kitu. Inaongoza kileleni kwa pointi 23 katika michezo tisa iliyocheza kati ya hiyo imeshinda saba, imepata sare mbili, ikiwa na jumla ya mabao ya kufunga 17 na kuruhusu kufungwa matatu pekee. Timu hiyo inajivunia mchezaji wake Shizza Kichuya akiongoza katika safu ya ushambuliaji kwa kufunga mabao saba peke yake hadi sasa, huku wengine katika timu nyingine wakifunga kuanzia manne. Hiyo ni kabla ya matokeo ya jana. Iwapo itaendeleza ushindi itajiwekea rekodi ya kucheza michezo 10 bila kupoteza. Lakini pia, macho yataendelea kuwatazama washambuliaji wake wenye uchu wa kufunga wakati wote ambao ni Kichuya, Ibrahim Ajib na Laudit Mavugo. Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja alisema kuwa ikiwa kikosi chake kitaendeleza umoja ilionao sasa, basi njia itakuwa nyeup...
Comments
Post a Comment