MAJIMAJI YASAJILI MLINZI MAHILI KUTOKA SIMBA SC KWA MKOPO
![]() |
Simwanza kulia akiwania mpira |
Kufuatia kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha Simba, beki Emmanuel Simwanza ametolewa kwa mkopo katika klabu ya Majimaji.
Semwanza alisajiliwa mwanzoni mwa msimu huu akitokea klabu ya Mwadui lakini alishindwa kabisa kupata nafasi ya kucheza kutokana ushindani wa namba katika kikosi cha Simba.
Wakati huo, Majimaji wameshindwa kupata saini ya kiraka Mbuyu Twite licha ya awali kuwa katika nafasi nzuri ya kukamilisha mipango hio.
Inadaiwa Twite alighairi dakika za mwisho na kushindwa kutokea kufanya mazungumzo ya kuhimitisha mpango wa kuhamia Majimaji.
Comments
Post a Comment