MBEYA CITY FC YAIMARISHA SAFU YAKE YA USHAMBULIAJI
Kocha Kinnah Phiri wa Mbeya City ameamua kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kwa kuwachukua nyotawawili wa African Lyon, Hood Mayanja na Tito Okello.
Washambuliaji hao raia wa Uganda, walikuwa wachezaji muhimu katika kikosi cha African Lyon toka ikiwa Ligi Daraja la Kwanza.
Mbeya City inashikilia nafasi ya nane ikiwa na tatizo la ufungaji wa mabao baada ya kufunga mabao 13 tu katika mechi 15 ilizocheza msimu huu.
Comments
Post a Comment